Mwanamuziki mwanasiasa Bobi Wine ambaye amekuwa akizuiliwa kwa karibu wiki mbili nchini Uganda ameachiliwa huru kwa dhamana na Mahakama Kuu mjini Gulu, kaskazini mwa nchi hiyo.
Mbunge huyo wa Kyadondo Mashariki ambaye jina lake halisi ni Robert Kyagulanyi amepewa dhamana pamoja na wabunge wengine watatu, na watuhumiwa wengine wanane.
Washtakiwa hao wanadaiwa kuhusika katika kurushia mawe magari ya msafara wa Rais Yoweri Museveni wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa eneo bunge la Arua.
Kassiano Wadri aliyeshinda ubunge Arua ni miongoni mwa wabunge waliokuwazuiliwa.
Bw Wadri ameachiliwa kwa dhamana lakini akazuiwa kuzuru eneo bunge lake kwa miezi mitatu bila idhini ya mahakama.
Maombi ya dhamana ya washukiwa wengine 21 walioshtakiwa pamoja na Bobi Wine yatasikilizwa na mahakama baadaye leo.
Awali, taarifa zilikuwa zimesema kuwa wakili wa kimataifa aliyekuwa amepewa kazi ya kumwakilisha, Bobi Wine, amezuiwa kuingia nchini humo.
Gazeti la kibinafsi la the Monitor nchini humo limeripoti kuwa Robert Amsterdam ameorodheshwa kama mtu asiyetakikana nchini Uganda na serikali ya nchi hiyo.
Alikuwa miongoni mwa mawakili waliokuwa wameorodheshwa kumtetea Bw Kyagulanyi katika kesi ambapo ameshtakiwa uhaini.
Gazeti la kibinafsi la the Monitor nchini humo limeripoti kuwa Robert Amsterdam ameorodheshwa kama mtu asiyetakikana nchini Uganda na serikali ya nchi hiyo.
Title :
Bobi Wine: Mbunge na mwanamuziki nyota aachiliwa huru kwa dhamana Uganda
Description : Mwanamuziki mwanasiasa Bobi Wine ambaye amekuwa akizuiliwa kwa karibu wiki mbili nchini Uganda ameachiliwa huru kwa dhamana na Mahakama K...
Rating :
5